KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

Mgombea Chadema akamatwa akidaiwa kumtukana JK


Tumsifu Sanga

MGOMBEA ubunge wa Temeke kwa tiketi ya Chadema, Dickson Amas Ng’hilly jana alikamatwa na polisi na kuachiwa kwa dhamana.
Ng’hili, mwenye umri wa miaka 33, alikamatwa jana saa 4:00 asubuhi kwa kosa la kutumia lugha matusi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika juzi kwenye viwanja vya Mwembeyanga vilivyo Temeke jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa polisi wa Kanda ya Dar es salaam, Suleiman Kova alisema walimkamata Ng’hili na kumhoji kwa kosa la kutumia lugha ya matusi dhidi ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete.
Alisema mtuhumiwa alitoa lugha hiyo ilipofika zamu yake ya kujinadi baada ya kuruhusiwa na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa.

“Ilipofika zamu ya kutoa hotuba, Dickson Amos Ng’hili anatuhumiwa kutoa lugha ya matusi dhidi ya mgombea urais Jakaya Kikwete ambayo ni kinyume cha sheria chini ya kifungu namba 89 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 (Penal Code Cap.16 of the Laws)," alisema Kamanda Kova.

Mtuhumiwa ameandika maelezo yake ya utetezi kwa mujibu wa sheria na upelelezi bado unaendelea, alisema Kova.
Kamanda Kova aliongeza kuwa kwa kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, mtuhumiwa ameachiwa huru kwa dhamana ya polisi akisubiri matokeo ya uchunguzi huo.

Hazta hivyo, Kova hakutaka kutaja maneno yaliyotafsiriwa kuwa ni lugha ya matusi dhidi ya Kikwete, akisema kuwa hawezi kuyarudia na kwamba watapeleka mahakamani kutumika kama ushahidi.
Kova alisema mtuhumiwa alihojiwa kwa kufuata taratibu na tukampa uhuru wa kujitetea kwa kuwa naye anaweza kuwa na mashahidi wake na ndio maana tumempa dhamana wakati upelelezi unaendelea

No comments:

Post a Comment