KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, October 29, 2010

Kiharusi chaongoza Dar



IMEDAIWA kuwa wakazi waliowengi waishio jijini Dar es Salaam huongoza kwa kuugua ugonjwa wa kiharusi kuliko mikoa mingine nchini.


Hayo yamebainika katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya aTaifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu [NIMR] na kutolewa tathimini hiyo jana.

Akizungumza na wanahabari jana katika sehemu ya kuadhimisha siku ya ugonjwa huo, Dk. Gerry Mshana alsiema, jiji la Dar es Salaam linongoza kwa wagonjwa hao.

Alisema katika utafiti uliofanyika umebaini kuwa kati ya watu laki moja watapatikana watu 316 wana ugonjwa huo katika jiji hilo.

Alisema utafiti huo umefanyika umebaini kuwa mabadiliko ya maisha ni chanzo cha kuongezeka kwa agonjwa hao ambao chanzo chake ni shinikizo la damu na kupelekea apaate maradhi hayo.

Alisema dalili za ugonjwa huo ni pamoja na kupata ganzi ghafla mwilini na kuishiwa nguvu,kupata ugumu wa kuzungumza wa ghafla,kutoona vizuri kwa ghafla,kushindwa kutembea kwa ghafla ,kizunguzungu na kuumwa kichwa sana bila chanzo cha msingi.

Alisema idadi hiyo ya wagonjwa ni kubwa kuliko hata nchi zilizoendelea

No comments:

Post a Comment