KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, October 29, 2010

Atengwa na nduguze baada ya kubadili dini


KIJANA mmoja aliyetambulika kwa jina la Christopher [31] mkazi wa Mabibo jijini Dar es Salaam, amejikuta akiwa kwenye wakati mgumu kutokana na hali yake ya maradhi yanayomsumbua baada ya kutengwa na ndugu zake baada ya kubadili imani yake ya kidini.
Christopher hivi sasa anakabiliwa na maradhi ya tumbo na kupelekea kulazwa katika zahanati moja binafsi, amejikuta akikosa huduma za ndugu zake na kuhudumiwa na upande wa mke wake pekee hali inayomfanya akose amani .

Imedaiwa na mmoja wa ndugu wa mke wake kuwa, Christopher alichukua umauzi wa kubadilisha imani yake ya kidini ili aweze kufunga ndoa na mchumba wake hali hiyo ilipokelewa kwa mitazamo tofauti na kutoka ndani ya familia yake.

Ilidaiwa kuwa, kijana huyo baaddhi ya ndugu hawakuafiki kitendo hicho cha kubadili imani kwa kuwa ndugu hao walitaka mke wake aje katika imani ya ndugu yao na si ndugu yao kubadili imani.

Hivyo imendelea kudaiwa kuwa, mke wake huyo aligoma kubadili dini na kwa kuwa kijana huyo hakutaka amkose mchumba wake huyo aliamua abadili ili aweze kufunga nae ndoa.

Imedaiwa kuwa kijana huyo alifunga ndoa na mke wake huyo mwezi Februari, mwaka huu na kuhudhuriwa na baadhi ya ndugu na hivi sasa anakabiliwa na maraadhi ya tumbo na ndugu kumsusa kwa kutompa ushirikiano katika kumuuguza.

Imedaiwa kuwa kijana huyo anatakiwa apatiwe upasuaji

No comments:

Post a Comment