KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, September 29, 2010

Watano Wafariki Katika Mashindano ya Kunywa Pombe




Watu Watano wamefariki wakati wakishindana kunywa pombe katika mji mmoja kaskazini mwa Msumbiji.
Watu watano wafanyakazi wa kiwanda kimoja cha bia nchini Msumbiji wamefariki wakati wakishandana na atamaliza mapema kunywa chupa tano za pombe kali.

Wanaume hao walifariki katika mashindano ya kunywa pombe yaliyofanyika kaskazini mwa Msumbiji, shirika la habari la Msumbiji la Noticias lilisema.

Vifo vya wanaume hao vilitokea katika hatua tofauti za mashindano hayo ya kunywa kwa haraka chupa tano za bia mpya ya kiwanda cha bia cha mji wa Nampula.

Polisi wametoa taarifa ya tukio hilo ikiwa ni mwezi mmoja baada ya tukio hilo kutokea katika mji wa Alto Molocue.

Taarifa zilisema kuwa vifo vya wanaume hao ambao walikuwa ni wafanyakazi wa kiwanda kilichotengeneza bia hizo, vilitokea wakati wa promosheni ya kuzitangaza bia hizo.

Baadhi ya washiriki walifariki punde tu baada ya kupiga fundo chache za bia hiyo, liliripoti gazeti la Noticias.

Mkuu wa mkoa wa Alto Molocue ameanzisha uchunguzi kuhusiana na vifo hivyo

No comments:

Post a Comment