KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, September 13, 2010

Mfumo wa magereza ya Irak wakosolewa



LONDON

Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International, limechapisha ripoti hii leo likisema watu takriban 30,000 nchini Irak


wamehukumiwa vifungo gerezani bila kufunguliwa mashtaka wala kuwa na wakili. Shirika hilo linasema wafungwa wanakabiliwa



na kitisho kikubwa cha mateso na kutendewa vitendo vibaya.




Kwa mujibu wa ripoti hiyo shirika la Amnesty International linasema maafisa wa Irak wanawazuilia wafungwa wasio rasmi




katika magereza ya siri na watu kadhaa wamekufa kutokana na mateso gerezani. Katika ripoti hiyo, iliyopewa jina "Enzi mpya ya utawala





mateso yale yale" shirika hilo linaitaka serikali ya Irak kuwalinda vyema zaidi wafungwa.

No comments:

Post a Comment