KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, June 8, 2010

Wawili wafa mashindanoni Rwanda


Watu wawili wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa nchini Rwanda wakati gari lilipopenya kwenye mkusanyiko wa washangiliaji katika mashindano ya magari.

Dereva ambaye ni raia wa Kenya ameripotiwa kupoteza njia alipokuwa akiendesha gari hilo kwa kasi kubwa siku ya Jumapili usiku.

Wawili miongoni mwa waliojeruhiwa wako katika hali mbaya sana.

Mashindano ya magari ya KCB Mountain Gorilla yanayofanywa mashariki mwa wilaya ya Gatsibo yaliandaliwa kusherehekea siku ya mazingira duniani.

No comments:

Post a Comment