KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, June 26, 2010

WATU saba wa familia moja wamekufa baada ya kuteketea kwa moto


WATU saba wa familia moja wamekufa baada ya kuteketea kwa moto uliozuka ghafla usiku katika nyumba waliyokuwa wakiishi huko maeneo ya Soweto mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya. Bw. Nyombi alisema chanzo cha awali kutoka jeshi la polisi kilibaini, moto huo uliwashwa na mtoto wa mwenye nyumba hiyo kwa makusudi kutokana na chuki aliyolimbikiza kwa baba yake kwa kuwa alimuacha mama yake na kuoa mke mwengine.

Moto huo ulizuka usiku wa kuamkia jana ulioanza majira ya saa 5:00 usiku baada ya nyumba hiyo kumwagiwa mafuta ya petrol na kuwashwa moto baada ya watu wote wakiwa wameshaingia ndani kwa ajili ya kulala.

Hata hivyo zimamoto ilipofika mahali hapo walikuta miili hiyo ipo katika hali mbaya na walikuaw wakijitahidi moto usifike katika nyumba nyingine ili usiweze kumaliza watu werngi zaidi.

Hivyo miili hiyo ilichukuliwa na kwenda kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Kamanda Nyombi alisema chanzo cha moto huo kinaendelea kuchunguzwa zaidi mbali na hiyo iliyotolewa awali na mtoto huyo anashikiliwa na polisi.

Waliokufa katika tukio hilo ni baba mwenye nyumba hiyo Daniel Mwang’ombe (75) Anita Richard (46) mke ,Salome Mwang'ombe (18).

Wengine ni Diana Samson (18), Jane Samson, Claud na msichana wa kazi aliyefahamika kwa jina la Mariam

No comments:

Post a Comment