KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, June 29, 2010

Mwaupulo aahidi kuteketeza changamoto zinazoikabili jimbo la Kawe


KIJANA Undule Hezron Mwampulo[34] ametangaza nia ya kugombea kiti cha Ubunge katika jimbo la Kawe kwa tiketi ya [CCM] ili kuweza kukabiliana na changamoto zinazoikabili jimbo hilo kwa muda mrefu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, jijini Dar es Salaam, Mwampulo amesema amejitokeza kuwania kiti hicho ili kukabiliana na matatizo sugu ya jimbo hilo.

Amesema lengo lililomvutia kuwania kiti hicho ni kuguswa na matatizo ya muda mrefu yasiyotekelezeka yakiwemoya huduma za afya, maji, elimu.

Amesema kubwa ya yote ni kutaka kumaliza matatizo ya ardhi yanayoikabili jimbo hilo na kuahidi matatizo hayo atayatatua.

MBali na hilo amesema wananchi wa jimbo hilo wamekuwa wakilalamikia ana matatizo ya usafiri, pia miundombinu mibovu hjaa katika kata ya Msasani.

Hivyo amesema kutokana na kero hizo zilizodumu kwa muda mrefu atahakikisha atamaliza matatizo hayo kwa kutumia uzoefu wake wa kielimu kumaliza matatizo ya jimbo hilo.

Mwampulo amesema ametangaza nia hiyo kutokana na kuvutiwa na wito wa Rais Kikwete ya kuwataka vijana warudi nyumbani kuendeleza nchi yao.

Mwampulo ameitikia wito huo wa rais na amerudi nyumbani akitokea nchini Uingereza alipokuwa akiendesha shughuli zake na kupata degree mbalimbali akiwa nchini humo.

No comments:

Post a Comment