KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, June 22, 2010

His-bal Islam waondoka Beledweyne

Kundi la wapiganaji wa Kiislami, la Hisb al-Islam, nchini Somalia, limetangaza kuwa wapiganaji wake wameondoka kwa hiari kutoka mji wa Beledweyne ulioko kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishi.


Kiongozi wa kundi hilo Sheikh Hassan Dahir Aweys amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kuzuia makabiliano kati ya wapiganaji wake na wale wa kundi la Al Shabaab.

Wakati huo huo Aweys ametoa wito wa maridhiano kati ya makundi hayo mawili.

Msemaji wa kundi hilo ameiambia bbc kuwa wapiganaji wake wanaendelea kujiodnoa kwenye kundi hilo na kujiunga na kundi hasimu la al-Shabaab.

No comments:

Post a Comment