KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Unyumba Kila Siku Wasababisha Aione Ndoa Chungu


MWANAMKE mmoja [jina kapuni] amelazimika kuchukua maamuzi ya kuchelewa kurudi nyumbani kwake kutoka kazini ili kukwepa kumpa unyumba mumewe ambaye anadaiwa kutumia dawa za kimasai za kuongeza nguvu za kiume.
Mwanamake huyo ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya utengenezaji wa vinywaji vya cocacola,amekutwa na kadhia hiyo ambayo hajui itamuisha lini ambayo amesema inamkosesha raha ya maisha ya ndoa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, mwanamke huyo alisema kuwa mume wake amebadilika kitabia na amezidisha unywaji wa pombe.

Mwanamke aliendelea kusema kuwa mumewe anapolewa huwa mkorofi kupita kiasi.

Kubwa ya yote amesema kuwa anafanya maamuzi ya kuchelewa kurudi nyumbani kwake sasa hivi kwa kuwa mume wake huyo amekuwa akionekana kupenda zaidi unyumba tofauti na miaka ya nyuma hali inayofanya achoshwe na zoezi hilo.

“Sikia yaani nilivyochoka hapa ngoja nikaekae hapa hadi masaa yaende kwanza, nikirudi nitamkuta ameshalala hataulizia tena mana nisikufiche nimechoka kila siku nakandamizwa inachosha”

Amedai kuwa akiwahi kurudi tu na kumkuta mumewe amesharudi basi ni kazi moja tu hadi uchwao.

Hata hivyo alidai kuwa huenda anahisi mume wake anatumia vilevi ama hizo dawa za kimasai zinazofanya awe na nguvu kupita kiasi hali ambayo inampa shida na kutamani kuchelewa kurudi nyumbani kwake.

Amesema ameishaishi na mume wake huyo kwa miaka sita sasa na wamebahatika kupata watoto wawili mapacha wa kike na kiume ambao kwa sasa wana umri wa miaka miwili na nusu.

No comments:

Post a Comment