KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, May 11, 2010

Nigeria Yatangaza Kikosi cha Kombe la Dunia


Tuesday, May 11, 2010 3:27 AM
Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles ametangaza kikosi cha wachezaji watakaoiwakilisha Nigeria kwenye kombe la dunia mwezi ujao nchini Afrika Kusini bila ya kumsahau mtu mzima Nwanko Kanu.
Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria Lars Lagerback ambaye alikabidhiwa mikoba ya ukocha wa Nigeria baada ya kocha Shaibu Amodu kuvurunda kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Angola, ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji 30 ambacho baadae kitachujwa na kubaki na wachezaji 23 watakoiwakilisha Nigeria kwenye fainali za kombe la dunia zinazoanza mwezi ujao.

Katika kikosi hicho Lars amemuita nyota wa Portsmouth ya Uingereza iliyoshuka daraja, mkongwe Nwanko Kanu.

Magolikipa watatu kati ya wanne walioitwa na kocha wa Nigeria wanacheza soka nchini Israel.

Kikosi kamili cha Nigeria ni kama ifuatavyo:

Magolikipa: Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv, Israel), Dele Aiyenugba (Bnei Yehuda, Israel), Austin Ejide (Hapoel Petah Tikva, Israel), Bassey Akpan (Bayelsa United, Nigeria)

Mabeki: Taye Taiwo (Marseille, France), Elderson Echiejile (Rennes, France), Chidi Odiah (CSKA Moscow, Russia), Onyekachi Apam (OG Nice, France), Joseph Yobo (Everton, England), Daniel Shittu (Bolton Wanderers, England), Ayodele Adeleye (Sparta Rotterdam, Netherlands), Rabiu Afolabi (SV Salzburg, Austria), Terna Suswan (Lobi Stars, Nigeria)

Viungo: Chinedu Ogbuke Obasi (TSG Hoffenheim, Germany), John Utaka (Portsmouth, England), Brown Ideye (FC Sochaux, France), Peter Utaka (Odense Boldklub, Denmark), Kalu Uche (Almeria, Spain), Dickson Etuhu (Fulham, England), John Mikel Obi (Chelsea, England), Sani Kaita (Alaniya, Russia), Haruna Lukman (AS Monaco, France), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev, Ukraine), Osaze Odemwingie (Lokomotiv Moscow, Russia)

Washambuliaji: Yakubu Aiyegbeni (Everton, England), Victor Anichebe (Everton, England), Nwankwo Kanu (Portsmouth, England), Obafemi Martins (Wolfsburg, Germany), Ikechukwu Uche (Real Zaragoza, Spain), Victor Obinna Nsofor (Malaga, Spain)

No comments:

Post a Comment