KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, May 29, 2010

Mzee Pwagu Afariki Dunia


Muigizaji mahiri nchini Tanzania, Rajab Kibwana Hatia au maarufu kwa jina la Pwagu ambaye alitamba sana redioni kwenye mchezo wake wa Pwagu na Pwaguzi, amefariki dunia jana akiwa na umri wa miaka 87.
Mzee Pwagu alifariki jana ijumaa kwenye hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam baada ya kuugua muda mrefu maradhi ya uzeeni.

Mzee Pwagu alitamba sana redioni kwenye miaka ya 60 hadi 80 katika kipindi cha redio kilichokuwa kikirushwa hewani na redio ya taifa Redio Tanzania Dar Es Salaam (RTD) akimshirikisha rafiki yake Ali Said Keto ambaye yeye alikuwa maarufu kwa jina la Pwaguzi.

Mzee Pwagu ambaye alizaliwa mwaka 1923 mjini Tabora atakumbukwa zaidi kwa juhudi zake za kuinua sanaa za maigizo nchini.

Mzee Pwagu ndiye aliyekuwa muanzilishi wa kundi la Kaole ambalo limetoa wasanii wengi wanaotamba hivi sasa kwenye anga la filamu Tanzania kama vile Ray na Kanumba.

Mazishi ya Mzee Pwagu yatafanyika leo kwenye makaburi ya Kigogo jijini Dar es Salaam.

MUNGU AMLAZE MZEE PWAGU MAHALI PEMA PEPONI -- AMEN

No comments:

Post a Comment