KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, May 11, 2010

Mwanamke Afanya Mapenzi na Mbwa, Nguruwe na Punda


Mwanamke mmoja nchini Marekani amefikishwa mahakamani kwa kufanya mapenzi na wanyama mbali mbali kama vile nguruwe, mbwa na punda na pia anakabiliwa na kesi ya kuwaambukiza wanyama magonjwa ya zinaa.
Dovie Lee Kerner, mwanamama mwenye umri wa miaka 47 wa mji wa Plumville, Pennsylvania nchini Marekani anakabiliwa na mashtaka ya kuwaambukiza magonjwa ya zinaa wanyama na binadamu.

Inadaiwa kuwa Dovie ambaye anaishi na mpenzi wake ana pepo kali sana la ngono kiasi cha kutochagua mwanaume yupi au mnyama yupi wa kufanya naye mapenzi.

Dovie anakabiliwa na kesi ya kufanya mapenzi na punda, mbwa na nguruwe.

Polisi wa Pennsylvania waligundua mchezo mchafu wa Dovie baada ya mpenzi wake kuwapigia simu polisi na kuuliza kama kufanya mapenzi na wanyama ni kosa.

Polisi walipomwambia kuwa ni kosa kubwa kufanya mapenzi na wanyama, mpenzi wake huyo aliwaambia polisi kuwa anayo video ya mpenzi wake akifanya mapenzi na mbwa, punda na nguruwe.

Polisi hapo hapo walimtia mbaroni Dovie ambaye kutokana na mchezo wake huo wa kufanya mapenzi na wanyama alimuambukiza mbwa gonjwa la zinaa ambalo polisi hawakulitaja.

Dovie pia anadaiwa kumwambukiza mpenzi wake huyo gonjwa hilo la zinaa.

Dovie amefunguliwa mashtaka ya ukatili kwa wanyama na atafikishwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa.

No comments:

Post a Comment