KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Ampa Mimba Binti Yake, Amuua Akijaribu Kuitoa


Mwanaume mmoja nchini Jordan anashikiliwa na polisi baada ya kumuua binti yake wakati alipojaribu kuitoa mwenyewe mimba aliyompachika.
Mwanaume mmoja nchini Jordan anashikiliwa na polisi kwa makosa ya kumbaka binti yake na kusababisha kifo chake alipoamua kuitoa mimba aliyompachika.

Taarifa ya polisi ilisema kwamba mwanamke mwenye umri wa miaka 19 alifariki dunia siku ya jumapili baada ya kupoteza damu nyingi sana wakati baba yake alipoamua kuitoa mwenyewe mimba aliyompachika.

Taarifa ya polisi haikusema baba huyo alitumia njia gani kuitoa mimba hiyo ya binti yake ambayo ilikuwa na umri wa miezi mitano.

Msemaji wa polisi alisema kwamba tukio hilo lilitokea kwenye mji wa Zarqa kaskazini mashariki mwa Jordan.

Baba huyo ambaye ana umri wa miaka 46 amekiri kuwa alikuwa akifanya mapenzi na binti yake kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita na pia alisema kuwa mama wa binti huyo alikuwa akijua kinachoendelea.

Amefunguliwa mashtaka mashtaka matatu ya mauaji, ubakaji na utoaji mimba.

Baba huyo huenda akahukumiwa adhabu ya kifo iwapo mahakama itamuona ana hatia.

Haijajulikana kama mama wa binti huyo naye atapandishwa kizimbani kwa kuifumbia mambo tabia mbaya ya mume wake.

No comments:

Post a Comment