KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, March 3, 2010

Al Shabaab wafurusha wafanyikazi wa WFP, Somalia

Kundi la wapiganaji wa kislamu nchini somalia, Al-shabaab, wameamrisha shirika la Umoja wa Mataifa wa mpango wa chakula, WFP, kusimamisha shughuli zake na kuondoka nchini humo.

Kundi hilo linalodhibiti maeneo mengi ya kusini mwa nchi hiyo, limesema kuwa litachukua hatua dhidi ya raia yeyote wa Somalia anayeshirikiana na shirika hilo la WFP.

Kundi hilo limesema WFP linaangamiza wakulima nchini humo kwa kusambaza chakula cha bure nchini humo.

No comments:

Post a Comment