KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Togo yakata rufaa




Shirikisho la soka nchini Togo limekata rufaa katika mahakama ya usuluhishi ya mpira wa miguu (CAS) baada ya nchi hiyo kupigwa marufuku kushiriki mashindano mawili ya kombe la Afrika.
Adhabu hiyo ilitolewa baada ya Togo kujiondoa katika mashindano ya hivi karibuni nchini Angola.

Kujitoa kwao kulitokana na kushambuliwa na bunduki ambapo watu wawili wa timu ya Togo waliuawa.

Shirikisho la soka barani Afrika (caf) limesema, serikali iliingilia kati masuala ya soka kutokana na hatua ya waziri mkuu wa Togo kuitaka timu hiyo kurudi nyumbani.

Mkuu wa kamati ya mpito ya tume inayoshughulikia mpira Togo, Jenerali Seyi Memene amesema jopo la wanasheria wameteuliwa kuisimamia kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment