KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, January 21, 2010

Rais Barack Obama amekiri kuwa wamarekani hawajaridhishwa na hatua za serikali yake


Nisamehe niliteleza, Obama anadi wamarekani

Rais Barack Obama amekiri kuwa wamarekani hawajaridhishwa na hatua za serikali yake mwaka mmoja baada ya kumchagua.
Katika mahojiano ya kuadhimisha mwaka mmoja madarakani, Obama amesema kuwa atawasikiza zaidi wananchi wake na kushughulikia malalamiko yao.

Alikuwa akizungumza siku moja baada ya chama chake kupoteza kiti muhimu zaidi cha senate katika jimbo la Massachusettes na hivyo kutikisa siasa za nchi hiyo.

Obama ambaye ameshutumiwa kwa kusisitiza juu ya mabadiliko ya sekta ya afya na kusahau kuongeza ajira na kuinua uchumi, sasa ameahidi kupunguza joto kwa mswada wake wa afya.

No comments:

Post a Comment