KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Sunday, January 10, 2010

Didier Drogba mwanasoka bora Afrika




Didier Drogba wa Chelsea na Ivory Coast ametangazwa mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa BBC Afrika 2010.
Mshambuliaji huyo amepata kura zaidi kuliko Samuel Eto'o, Michael Essien, Yaya Toure, na Tresor Mputu Mabi kushinda taji hilo.

Matokeo ya kura - zilizopigwa na mashabiki kote Afrika yalitangazwa moja kwa moja kutoka Angola kupitia kipindi cha Fast Track katika Idhaa ya Kiingereza ya BBC.

Drogba yupo Angola akiiongoza nchi yake kujiandaa kwa michuano ya kombe la mataifa ya Afrika, ambako The Elephants wanapewa nafasi kubwa ya kushindwa.

Baada ya kuanza mwaka vibaya, Drogba aliimarisha kiwango chake cha soka na kuwa mmoja wa washambuliaji tishio duniani.

Baada ya kuwekwa kando kucheza kikosi cha kwanza na kocha Luis Felipe Scolari kutoka Brazil, mshambuliaji huyo alifunga goli moja tu katika mechi 10 ilipofika Februari.

No comments:

Post a Comment