KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Sunday, December 27, 2009

Waisrael wauwa Wapalestina sita


Hiki ni kizazi cha baba wetu wa imani kinachopambana wenyewe kwa wenyewe kwa msaada wa nchi za magharibi na marekani.
mpaka sasa Tatizo la kizazi cha wana Wa Nabii Ibrahimu limekuwa janga na maslahi kwa baadhi ya watu Duniani.

Kizazi cha Israel au nabii Jakubu ndicho kizazi Kinachotokana na Mtoto wa Pili wa Ibrahimu ambae ni Isihaka (Isack) na kizazi cha Warabu kinatokana na mtoto wakwanza wa Nabii Ibrahimu, ambae ni Ismail.

Tatizo la wapalestina na waisrael lina misingi miwili mikubwa duniani, ambayo ni Dini na Siasa katika umiliki wa ardhi.

Waisrael wauwa Wapalestina sita

Wanajeshi wa Israeli wamewauwa Wapalestina sita, watatu katika ukanda wa Gaza na wengine watatu katika Ukingo wa Magharibi.

Msemaji wa Israel ameliambia shirika la habari la Uingereza la Reuters kuwa Wapalestina watatu waliouwawa Gaza ni kutokana na shambulio la anga.


Katika Ukingo wa Magharibi, wanajeshi wa Israel wanaarifiwa kuwapiga risasi na kuwauwa Wapalestina watatu katika mji wa Nablus.


Mashambulio hayo yametokea siku mbili baada ya raia mmoja wa Israel kuuwawa katika shambulio la kuvizia katika Ukingo wa Magharibi.

No comments:

Post a Comment