KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Sunday, December 27, 2009

Kenya yafuta Polisi 88





Taarifa kutoka Kenya zinasema serikali imewafuta kazi maafisa 88 wa Polisi kwa kukiuka taratibu za serikali.

Radio ya shirika la utangazaji la Kenya KBC imemnukuu afisa wa ngazi za juu katika Polisi Bwana Kinuthia Mbugua , akisema uamuzi huo umechukulia ili kurekebisha hadhi ya kikosi cha Polisi na kuwapa watu imani.

Bwana Mbugua ameripotiwa kusema kwamba umma umepoteza imani na Polisi kutokana na tabia ya maafisa wanaokiuka sheria.


Amesema wakuu wa Polisi wanajaribu kwa kila njia kurejesha heshima ya kikosi cha Polisi nchini Kenya.

No comments:

Post a Comment