KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, December 8, 2009

Ntaganda akanusha kushirikiana na FLEC


Ntaganda akanusha kushirikiana na FLEC

Huku maafa yakiendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Bosco Ntaganda amekana madai ya kushirikiana na kundi jingine la waasi.
Ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa inasema kundi linaloongozwa na Bosco Ntaganda linalowasaka waasi wa FDLR huenda likawa tishio kubwa mashariki mwa Congo.

Bosco Ntaganda amekanusha madai ya umoja wa mataifa kuwa, anashirikiana na kundi la waasi lijulikanalo kama Front for the Liberation and Emancipation of the Congo (FLEC).

Bw Ntaganda amekanusha madai hayo katika mahojiano aliyofanya na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.


No comments:

Post a Comment