KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 25, 2009

Ripoti: Wajanja wageuza yatima biashara


Ripoti mpya inaeleza kuwa watoto wanne kati ya watano wanaoishi katika makazi ya yatima kote duniani wana mzazi angalau mmoja.
Shirika la hisani la kusaidia watoto la Save the Children, limesena baadhi ya taasisi zinawarubuni wazazi masikini kuwatoa watoto wao.

Matokeo yake, ripoti inasema, maisha ya mamilioni ya watoto yako hatarini kwa kuishi katika nyumba za yatima, na wanakabiliwa na ubakaji, kutoroshwa nje ya nchi na vipigo.

Save the Children inasema misaada inatakiwa kuelekezwa katika miradi inayosaidia familia kuwatunza watoto wao.

Ripoti inadai viituo vya kutunzia yatima imegeuka kuwa biashara kubwa katika baadhi ya nchi, ambao wanaoviendesha hupokea msaada wa kifedha kutoka serikali na wahisani wenye nia njema.

No comments:

Post a Comment