KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 25, 2009

Rais Obama akusudia kumaliza kazi Afghanistan


Rais Obama akusudia kumaliza kazi Afghanistan

WASHINGTON




Rais Barack Obama wa Marekani amesema anakusudia kumaliza kazi nchini Afghanistan wakati akijiandaa kutangaza uamuzi wake mpya kuhusu mkakati wa nchi yake nchini humo, wiki ijayo. Kamanda wa Marekani, Stanley McChrystal alitoa ombi kwa Rais Obama la kuidhinisha wanajeshi elfu 40 zaidi kupelekwa Afghanistan kwa ajili ya kupambana na wanamgambo wa Taliban.

Uamuzi wa Rais Obama unaosubiriwa kwa muda mrefu huenda ukabadili sera za washirika wake katika Jumuiya ya Kujihami ya NATO. Kuna taarifa kuwa Rais Obama atapeleka kati ya wanajeshi 30,000 na 40,000 zaidi nchini Afghanistan. Kwa sasa Marekani ina wanajeshi 68,000 nchini humo kati ya wanajeshi 110,000 wanaoongozwa na NATO.

No comments:

Post a Comment