KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Rais wa Nigeria aumwa maradhi ya moyo


Rais Umaru Yar'Adua wa Nigeria ana matatizo ya moyo, msemaji wake ameeleza, baada ya kusafirishwa kwenda Saudi Arabia siku ya Jumatatu kupata matibabu.
Bw Yar'Adua ana maradhi yajulikanayo kama pericarditis, au kiungulia kuzunguka moyo wake, msemaji wake ameieleza BBC.

Alisema kuwa rais huyo, mwenye umri wa miaka 58, anaendelea vyema baada ya kuanza kutibiwa. Maafisa walikanusha taarifa za awali kwamba rais Yar'Adua alikuwa katika hali mahututi.

Bw Yar'Adua amekuwa na maradhi yasiyopona ya figo kwa miaka takriban 10.

Amekuwa akishindwa shughuli kadhaa za kiserikali kutokana na afya yake kumsumbua mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment