KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Mafuriko yaua watu 77 Saudi Arabia


Mafuriko huko Saudi Arabia yameua watu 77 na wengine wengi hawajulikani waliko baada ya mvua kubwa ambayo haijatokea kwa miaka mingi kunyesha.
Hakuna mtu hata mmoja aliyekufa ambaye ni miongoni wa mamilioni ya watu kutoka sehemu mbali mbali dunia ambao wanafanya Hajj, msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya Saudi alieleza.

Mvua nzito zinazoambatana na kimbunga zilinyesha siku ya Jumatano na kuchelewesha kuanza kwa shughuli za Hajj za kila mwaka katika mji mtukufu wa Makka.

Watu waliokufa kwa mafuriko walikuwa katika mji wenye bandari wa Jeddah, Rabigh na Makka, kwa mujibu wa shirika la habari la serikali - Saudi Press Agency.

No comments:

Post a Comment