KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 25, 2009

Mlinzi wa klabu ya Liverpool ya Uingereza, Jamie Carragher, ameelezea kwamba ikiwa timu yake itaondolewa katika mashindano ya klabu bingwa barani Ulay


Mlinzi wa klabu ya Liverpool ya Uingereza, Jamie Carragher, ameelezea kwamba ikiwa timu yake itaondolewa katika mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya, hili halitakuwa ni tatizo kubwa, kwani bado kitakuwemo katika ligi ya Europa.
Liverpool inahitaji Jumanne jioni kuishinda Debrecen ya Hungary, na ikitazamia pia wapinzani wao wakuu katika kundi la E, Lyon ya Ufaransa, watafanikiwa kuishinda Fiorentina ya Uhispania.

La sivyo, Liverpool haitafanikiwa kujiunga na timu 16 ambazo zitaendelea kuwepo katika mashindano.

Carragher alisema: "Bado tunaamini kwamba tunaweza kuendelea katika ligi ya klabu bingwa. La sivyo, tutaangazia yanayokuja".

"Klabu hakitakufa kwa kuondolewa kutoka ligi ya klabu bingwa".

No comments:

Post a Comment