KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 4, 2009

Mlinzi wa Arsenal Clichy aumia


Mlinzi wa Arsenal Gael Clichy hatocheza kwa wiki kadha baada ya kupata maumivu ya mgongo.
Clichy anayechezea nafasi ya ulinzi wa kushoto, alicheza siku ya Jumamosi ambapo Arsenal iliilaza Tottenham mabao 3-0, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi.

Kieran Gibbs atachukua nafasi yake katika mechi ya Jumatano ya ligi ya mabingwa wa Ulaya watakapochuana na AZ Alkmaar.

Maumivu hayo yanaweza pia kumkosesha Clichy kuwemo katika timu yake ya taifa ya Ufaransa kutafuta nafasi ya Kombe la Dunia, watakapomenyana na Ireland tarehe 14 mwezi wa Novemba mjini Dublin na siku nne baadae mjini Paris.

No comments:

Post a Comment