KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 11, 2009

Liverpool chupuchupu kulazwa


Mkwaju wa penalti ulioonekana na utata, uliopigwa na Steven Gerrard umeiokoa Liverpool na kwenda sare ya mabao 2-2 na Birmingham.
Gerrard alifunga penalti hiyo baada ya David Ngog kuonekana kujiangusha baada ya kukabiliwa na Lee Carsely.

Ngog mapema aliifungia bao la kwanza Liverpool, lakini mshambuliaji wa Barmingham Christian Benitez akasawazisha kwa kichwa muda mfupi.

Alikuwa mshambuliaji Cameron Jerome aliyeipatia bao la pili Birmingham, kabla Gerrad kusawazisha kwa mkwaju wa penalti.

Birmingham walimjia juu mwamuzi Peter Walton kwa kuipatia Liverpool penalti hiyo wakidai Ngog hakuguswa na Carsley.

No comments:

Post a Comment