KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, November 23, 2009

Henry anafikiria kuacha timu ya taifa


Thierry Henry anafikiria kuacha soka ya kimataifa kufuatia kuushika mpira wakati Ufaransa walipocheza na Jamhuri ya Ireland kuwania nafasi ya Kombe la Dunia.
Mshambuliaji huyo amejikuta katika mzozo mkubwa kutokana na kitendo chake hicho ambacho kiliisaidia Ufaransa kuitoa Ireland na kujipatia nafasi kwenda Afrika Kusini.

Alipoulizwa iwapo anafikiria kustaafu kufuatia utata uliojitokeza wa bao la kusawazisha dhidi ya Ireland, Henry alilieleza gazeti la Ufaransa la L'Equipe: "Ndiyo".

Chama cha soka cha Ireland kiliandika barua kwa Fifa wakitaka warudiane na Ufaransa.

Maombi hayo yalikataliwa licha ya Henry kutoa taarifa akisema kurudiana na Ireland ndio suluhisho.

No comments:

Post a Comment