KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Fifa yalaumiwa kwa ubabe Afrika Kusini


Waandishi wa habari wa Afrika Kusini wamelishutumu shirikisho la soka la dunia kwa kuweka masharti magumu kuandika habari za kombe la dunia mwaka 2010.
Waandishi hao wanasema kulingana na masharti hayo, vibali vya waandishi vinaweza kufutwa endapo wataandika taarifa zinazolikosoa shirikisho hilo.

Wanaasema Fifa imekataa kufafanua swala hilo licha ya jitihada za mara kwa mara kutoka kwa waandishi.

Lakini Fifa imesema masharti hayo yameeleweka vibaya na hayatakwamisha uhuru wa waandishi wa habari.

Hata hivyo, Raymond Louw, msemaji wa jukwaa la wahariri wa Afrika Kusini lijulikanalo kama Sanef, ameieleza BBC kuwa Fifa ina maswali mengi ya kujibu.

No comments:

Post a Comment