KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Sunday, May 22, 2011

Kikwete aongoza mazishi ya Sheikh Yahya






VIONGOZI mbalimbali wa siasa na dini akiwamo Rais Jakaya Kikwete, jana walijitokeza kumzika mtabiri maarufu wa nyota Afrika Mashariki na Kati Sheikh Yahya Hussein aliyefariki dunia juzi.



Wakati viongozi wengine wakijitokeza msibani hapo tangu asubuhi, Rais Kikwete alishiriki msiba huo kwenye mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya Tambaza yaliyoko jijini Dar es Salaam saa 10:00 jioni.



Viongozi wengine wa siasa walioshiriki mazishi hayo jana ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mjumbe wa Nec Mkoa wa Dar es Salaam, Adam Madabida na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.

Kabla ya kupelekwa kuzikwa mwili wa marehemu ulipelekwa katika Msikiti wa Manyema Kariakoo, kuombewa kwa maandamano yaliyojumuisha maelfu ya watu, yaliyoanzia nyumbani kwake Magomeni Mwembechai saa 9:00 alasiri.
Baadaye mwili huo ulipelekwa katika Makaburi ya Tambaza kwa maziko huku ukiwa umebebwa na mamia ya watu waliojitokeza huku wakitembea kwa miguu.

Baada ya kufika katika makaburi, Rais Kikwete aliongoza umati wa watu kuuzika mwili wa marehemu.
Mzee wa upako ahudhuria
Baadhi ya viongozi wa kidini waliofika nyumbani kwa marehemu mapema asubuhi ni pamoja na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban bin Simba na Mchungaji Adamu Lusekelo, maarufu kwa jina la 'Mzee wa Upako'.

Akizungumza katika msiba huo, Sheikh Simba alisema taifa limepoteza mtu muhimu ambaye pengo lake haliwezi kuzibika kiurahisi.Alisema anamfahamu Sheikh Yahya Hussein siku nyingi na alikuwa mtu wa karibu sana kwake wakishauriana na kutiana moyo katika mambo mbalimbali.

"Hili ni pengo bwana, halizibiki leo wala kesho. Nilimtumia huyu (Sheikh Yahya) kama mshauri wangu wa karibu. Moja ya mambo niliyoyapenda kwake ni kusikiliza anavyosoma Qur'an," alisema Mufti Simba.Akizungumza msibani hapo jana, Mchungaji Lusekelo alisema alioteshwa katika ndoto kifo cha Sheikh Yahya siku moja kabla.

Alisema Mungu alimwotesha kwamba Sheikh Yahya kapanda daraja na alipozunduka kutoka usingizini, akawa anaitafakari na kesho yake saa tano asubuhi, alipigiwa simu kujulishwa msiba huo. "Niliooteshwa na Mungu kuhusu kifo hiki hivyo huyu rafiki yangu ataenda kulala sehemu aliyoandaliwa," alisema

Viongozi CCM, Chadema, CUF


Mwakilishi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Adam alisema marehemu Sheikh Yahya alikuwa mtu wa watu hivyo ni vizuri akaenziwa kwa uchapakazi wake.

Alisema taifa limempoteza mtu mashuhuri na hata kwa upande wa chama (CCM) pia kimepoteza kada wake kwani Sheikh Yahya alikuwa mkereketwa chama hicho siku zote., alisema kwa sababu marehemu alikuwa hapendi unafiki na chuki, ni vizuri vyama vya siasa vikamuenzi kwa kuacha siasa za chuki.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema Sheikh Yahya alikuwa mtu mnyenyekevu hivyo ni bora kila mtu amuenzi kwa matendo yake.Alitaka pia vyama vya siasa kuacha chuki baina yao ili kumuenzi Sheikh Yahya ambaye katika siku ya uhai wake hakupenda chuki na unafiki.

Masheikh wamlilia
Katika tukio jingine vilio na majonzi vilivyotawala msibani hapo jana viliwafanya baadhi ya masheikh kushindwa kusoma Qur'an.Hata hivyo habari zilizopatikana msibani hapo jana zimeeleza kuwa masheikh wengi walioshindwa kusoma Qur'an ni marafiki wa karibu wa marehemu.

Kila walipokuwa wakisoma, walikatizwa na kelele za vilio na simanzi kutoka kwa waombolezaji.Sheikh Yahya Hussein alifariki dunia juzi saa nne asubuhi katika Hospitali ya Mount Ukombozi alikopelekwa kwa matibabu, baada ya kuugua ghafla.










Death in Islam






Imam Malik Ibn Anas saw the Death Angel in his sleep, and the Imam asked him: " How much left for me to live?". The Angel pointed to his five fingers. Then the Imam asked him: " Does that mean 5 years, or 5 months, or 5 days ?". Before the Imam had a chance to get an answer back, he woke up.

The Imam went to someone who would interpret dreams. That man told him: " Imam Malik, when the Angel pointed to his five fingers he didn't mean 5 years or months or days, but the Angel meant that your question ' how much left for me to live' is among 5 matters that only Allah (SWT) knows about, and he recited the following verse from the Qur,an:


"" Verily, with ALLAH alone is the knowledge of the Hour. And HE sends down the rain,


and HE knows what is in the wombs.

And no soul knows what it will earn tomorrow, and no soul knows in what land it will die. Surely, ALLAH is All-Knowing, All-Aware. "" 31:34



When Caliph Haroon Al-Rashid got very ill, illness that caused his death, he told his staff to go a head and dig his grave so he can see it before he dies. After the grave was prepared, he asked to be carried to the grave . Upon arrival, the Caliph Haroon looked down into the grave and then looked up toward the sky and said: " O' whom (Allah) his rule never ends, have mercy on whom (Haroon) his rule has ended.

One day the Prophet (pbuh) visited the Cemetery along with some of his followers, and he said to them: " I long for my beloved ones?". His followers said: " Aren't we your beloved ones O' messenger of Allah ". The Prophet (pbuh) said: " you are my companions ". Then they say: " who are your beloved ones?". The Prophet said: " People come after you believed in me without seeing me ". they asked: " How would you know them on Judgment day even though you haven't seen them O' messenger of Allah?". The Prophet said: " My followers are gathered ' Ghurr'an Muhajjalin ' ".

(( Gurr'an means light on the forehead, and Muhajjalin means light on the feet, and what brings about this light is the Ablution 'Wudu' ))

One day the Prophet (pbuh) went to a boy's funeral and he found his mother weeping and he asked: " why are you crying ". The mother said: " O' messenger of Allah, is my son in Heaven or Hell?". The prophet replied:" O' slave of Allah, He (Allah) knows his status better than I do ".

The Prophet said: " The Believer's Soul turns into a Bird in Paradise ". (( The above Hadith means, that upon the Believers death, his Soul becomes a bird in Paradise until the Resurrection day, when Allah (SWT) returns all souls to its original bodies ))












No comments:

Post a Comment