KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 26, 2011

Birmingham yafuta safari ya Tanzania






Birmingham City


Birmingham City wameamua kufuta safari yao ya kwenda Tanzania.

City, ambao wameshuka daraja katika ligi kuu ya England msimu huu walikuwa wasafiri kwenda Tanzania kupambana na Simba ya Yanga katika mechi za kirafiki.

Hata hivyo watayarishaji walishindwa kuthibitisha utaratibu wa safari hiyo katika muda waliopewa.

Mabingwa hao wa kombe la Carling sasa wanatafuta nchi ya kwenda kucheza mechi za za kalba ya kuanza kwa msimu.








Waasi wa Libya wafungua ofisi Marekani








Bw Jeffrey Feltman

Waziri mdogo wa Marekani Jeffrey Feltman amesema waasi wa Libya wamekubali mwaliko wa kufungua ofisi mjini Washington.

Bw Feltman ni mwanadiplomasia mwandamizi wa Marekani kuwatembelea waasi hao kwenye mji wa Benghazi.

Marekani imesisitiza kwa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi kuachia madaraka, lakini haijawatambua moja kwa moja.

Ziara hiyo imefanyika baada ya ndege za majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato kufanya mfululizo wa mashambulio kwenye mji mkuu wa Libya, Tripoli, mashambulio mazito kutokea mpaka sasa.

Maafisa wa Libya walisema watu watatu walifariki dunia na wengi kujeruhiwa katika shambulio lililofanyika kwenye kambi za jeshi.

Nato ilisema imerusha mabomu kwenye ghala la magari lililopo karibu na ngome ya Bab al-Aziziya ya Kanali Gaddafi uliotumiwa na majeshi yake katika mashambulio iliyofanywa dhidi ya raia.

Hata hivyo, serikali ya Libya imeielezea kama kituo cha kuhifadhi vifaa vya jeshi na waliouawa ni raia.










Kongamano la G-8 kuanza nchini Ufaransa


Kongamano la G8



Viongozi wa dunia wanatarajiwa kukutana katika eneo Deauville nchini Ufaransa, kwenye kongamano la mataifa manane yenye utajiri mkubwa zaidi duniani G8.

Mkutano wa leo unatokea wakati kumeibuka mataifa mengine ambayo uchumi wake unakua kwa kasi na kuibua hoja ya ushawishi na umuhimu wa G8.

Hata hivyo wadadisi wamesema matuko ya hivi karibuni hususan harakati za mageuzi ya kidemokrasia katika nchi za Kiarabu na changamoto zinazokumba mradi wa nuklia wa Japan yameshinikiza kundi la mataifa hayo makuu kutoa mwelekeo.

Miongoni mwa ajenda ni kiwango cha kuthibiti taarifa zinazosambazwa kupitia mtandao, pamoja na mabadiliko ya tabia nchi.

Viongozi wa mpito katika nchi za Tunisia na Misri pamoja na Jumuiya ya nchi za Kiarabu wamealikwa ili kujadili mchakato wa kufanikisha utawala wa kidemokrasia katika nchi hizo.
Viongozi wa serikali wa kongamano la G8




Viongozi wa serikali wa kongamano la G8

Mapema mwaka huu watawala wa muda mrefu katika nchi za Misri na Tunisia waling'olewa madarakani kupitia mapinduzi ya kiraia hali iliyochochea maandamano ya raia kudai mageuzi katika nchi nyingi za Mashariki ya Kati.

Aidha mzozo unaokumba nchi ya Libya unatarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho cha siku mbili.Viongozi hao wamegawanyika huku Urusi ikikosoa vikali harakati za jeshi la NATO dhidi ya majeshi ya Kanali Muammar Gaddafi.

Muungano wa NATO unatekeleza operesheni zake chini ya azimio la Umoja wa Mataifa katika kuwalinda raia wakati wa makabiliano kati ya jeshi la Gaddafi na makundi ya waasi.



Gaddafi compound hit by Nato attack









An office building inside Muammar Gaddafi’s Tripoli compound has been destroyed early as Nato air strikes hit close to the base from where the Libyan leader is believed to be directing government strategy in the civil war.
At least two large missiles or bombs struck a multistorey building in Bab al-Aziziya, the sprawling complex in the centre of Tripoli, shortly after midnight. Another building, a ceremonial reception area where Gaddafi hosted a delegation from the African Union two weeks ago, was badly damaged.


The roof of the office building, which also housed a library in which Gaddafi liked to read according to an official, caved under the impact. The ground over a wide area was covered in shattered masonry, broken glass and metal, with pools of water forming between piles of rubble. Three hours after the blast, thick dust was still in the air when the foreign media was taken to the site.
Reports of light injuries from the blasts varied from none to 45. The Libyan leader’s location was not known.
Gaddafi’s supporters, who gather at Bab al-Aziziya nightly to act as human shields against Nato air strikes, climbed on the shattered building as chunks of masonry still fell. They waved loyalist green flags and chanted pro-Gaddafi and anti-Nato slogans.
Inside the second building, furniture, picture frames and chandeliers lay amid rubble and covered with dust. The South African president, Jacob Zuma, along with two other Africa presidents, held talks here with Gaddafi earlier this month on a peace proposal.
It was the second time Nato had struck inside the compound since its military campaign started. A missile hit another administrative building in the early days of the strikes, causing extensive damage.
In the early hours of Saturday, two missiles hit a site a few hundred metres from Bab al-Aziziya. Nato appeared to have targeted an underground bunker, which was visible from the craters caused by the missiles.
Three members of the US Senate armed service committee called on Sunday for more military intervention in Libya. Republican Lindsey Graham told CNN that Gaddafi “needs to wake up every day wondering: will this be my last?’”
Monday’s strike on Gaddafi’s compound followed two days of heavy assault on the besieged city of Misrata by government forces. Despite the Libyan government’s claims that troops had pulled back from the city, forces on the ground stepped up shelling and rocket fire following gains made on the ground by rebels.









Nato yaishambulia Libya usiku kucha







Mashambulio ya anga Libya

Takriban milipuko mikubwa mitano imeitikisa Tripoli usiku kucha, wakati harakati za majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato zikiendelea kwenye mji mkuu wa Libya.

Kwa usiku wa pili, mashambulio ya anga yalilenga ngome ya Bab al-Aziziya ya Kanali Muammar Gaddafi.


Nato inatekeleza azimio la umoja wa mataifa la kulinda raia wa Libya, kufuatia maandamano dhidi ya uongozi wa Kanali Gaddafi.

Lakini Urusi, ambayo haikuunga mkono azimio hilo, imesema uvamizi huo ni ukiukwaji wa umoja huo.

Mwandishi wa BBC Andrew North mjini Tripoli alisema mashambulio ya Jumanne usiku si makubwa kama yaliyofanyika Jumatatu usiku, lakini bado yalitikisa majengo eneo kubwa.

Moshi ulionekana kutanda kwenye mji huo.

Nato ilisema ngome hiyo ya Bab al-Aziziya imekuwa ikitumika kama kituo cha majeshi na magari ya kijeshi yaliyotumika kushambulia raia.

Lakini serikali ya Libya imesema Nato inajaribu kumwuua Kanali Gaddafi na mashambulio ya usiku yanawatisha raia wa Tripoli.











Matatizo yakithiri Burkina Faso


Burkina Faso ni nchi imetia hali ngumu tangu kuuawa kwa kiongozi wake aliyependwa, Thomas Sankara katika mapinduzi ya kijeshi miaka ishirini iliyopita.

Hata hivyo juhudi zote zilizochukuliwa na mrithi wake na vilevile wakati mmoja rafiki mkubwa, Blaise Compaore hazijazaa matunda yoyote.

Hali iliyopo wakati huu ya ghasia ilianza mwezi febuari mwaka huu kwa mfululizo wa majaribio ya kuipindua serikali, likiwemo lililofanywa na walinzi wa Rais na mara nyingi yakimalizika kwa ghasia za kupindukia.




Rais Compaore wa Burkina Faso

Akifahamu vyema uwezo wa walinzi wa Rais na ushahid ulio bayana wa jinsi wanavyoweza kusababisha mageuzi ya kiongozi, Rais Compaore hakusita kuitikia madai yao ya nyongeza ya mishahara.

Akionyesha shaka juu ya vuguvugu la mwamko ulioanzia Arabuni kusambaa hadi nchini mwake, kiongozi huyo alimfuta kazi mkuu wa majeshi na polisi kisha akafanya mabadiliko ya baraza lake la Mawaziri.

Alimchagua Waziri mkuu mpya ili kuleta mabadiliko katika serikali ya iliyohudumu kwa kipindi kirefu na kuonekana kama iliyochoka.

Mapema siku ya jumatatu, walimu kote nchini Burkina Faso walianza mgomo wa kudai marupurupu. Wanafunzi nao wakawaunga mkono walimu wao.

Katika mji mkuu Ouagadougou, imearifiwa kuwa wanafunzi walichoma tairi za magari barabarani na kusababisha uharibifu wa majengo.

wanafunzi walisababisha uharibifu

Makundi ya vijana waliojaa ghadhabu waliandamana katika miji minne mikubwa nchini humo ukiwemo wa pili kwa ukubwa, Bobo Dioulasso. Katika mji wa kusini wa Gaoua, shahidi mmoja wa tukio aliiambia BBC kuwa makao makuu ya chama tawala na mali kutoka makao ya Rais zilichomwa.

Kwa sasa walimu wamefikia mapatano na serikali ya Burkina Faso kumaliza mgomo.

Serikali imekubali kutimiza matakwa ya shirika la walimu la mishahara mkubwa zaidi.

Mapema wiki hii, mwandishi wa BBC katika mji mkuu aliarifu kuwa kundi jingine la askari liliingia mitaani likifyatua risasi angani. Safari hii wakidai mshahara sawa na ule waliopewa walinzi wa Rais.

Kwa mujibu wa mhariri wa idhaa ya Kifaransa ya BBC, Mahamat Adamou, idhaa iliyojulikana kama BBC Afrique, anasema kuwa ukizingatia msimamo wa jeshi ambalo hadi sasa halijawasilisha madai ya kisiasa na bado linamtii Bw.Compaore hana wasiwasi ya kupinduliwa.

Pamoja na hayo upinzani ni mlegevu, umegawanyika na umeshindwa kutumia fursa hii ya ghasia kuonyesha uwezo wake.

Kiongozi huyo ana sifa ya kushiriki mapinduzi yaliyomuwezesha kuingia madarakani kwa kumpindua rafiki yake na hivi kushika wadhifa wa Wizara ya Ulinzi kuna maana kwamba anaweza kuamuru vikosi kuzima aina yoyote ya fujo au jeuri kutoka kwa yeyote au kundi lolote.

No comments:

Post a Comment