KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, March 22, 2011

Makaazi ya Kanali Gaddafi yashambuliwa


Ndege zake za kijeshi, zimeshambulia makaazi ya Kanali Gaddafi mjini Tripoli na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye jengo moja.

Viongozi wa muugano wa majeshi hayo wanasema jengo lililoharibiwa lilikuwa linatumika kuamrisha majeshi ya Libya yanayopigana na waasi.

Waandishi wa habari wametembezwa kwenye eneo hilo lakini hakuna taarifa ikiwa maafa yalitokea baada ya shambulizi hilo.

Naibu mkuu wa jeshi la wanamaji wa marekani Bill Gortney anasema mashubulizi hayo hayaja mlenga kanali Gaddafi.



Televisheni ya Libya imeonesha maiti na magari ya kijeshi yaliyoteketea kwenye barabara ya kuelekea mji wa Benghazi, shina la wapinzani wa serikali

Msemaji wa serikali ameeleza kuwa watu 64 wameuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na mataifa ya magharibi, lakini hakuna njia ya kuthibitisha taarifa hiyo.

Awali afisa mkuu wa jeshi la Marekani, , Mike Mullen, alisema ndege kutoka Qatar zinapelekwa huko, kuwa tayari kushiriki katika operesheni dhidi ya Libya, na nchi nyengine piya zimetoa ahadi kusaidia.

Adimeri Mullen alieleza kuwa agizo la Umoja wa Mataifa, la kuzuwia ndege za serikali kuruka katika anga ya Libya, sasa limetekelezwa, na majeshi ya Kanali Gaddafi, katika mji wa Benghazi, unaodhibitiwa na wapinzani, sasa hayawezi kusonga mbele.

Alisema hakuona taarifa, kuwa raia wameuwawa.



mpinzani na bunduki yake karibu na Benghazi


Urusi imetoa wito kwa Uingereza, Ufaransa na Marekani, ziache kushambulia maeneo yasiyokuwa ya kijeshi, na kwamba raia wameshambuliwa.

Mkuu wa Jumuiya ya Kiarabu, Amr Moussa, amesema mashambulio yamekwenda mbali, kushinda lile lengo la kulinda tu anga ya Libya, ambavyo ndivo jumuiya yake ilivotaka.













Museveni alaani mashambulizi ya Libya




Museveni anasema nchi za magharibi zinabagua Libya na amependekeza mashambulizi yakome
Harakati za jamii ya kimataifa zinazoendela dhidi ya Libya zimekosolewa Rais Yoweri Museveni wa Uganda.

Katika tahariri yake kuhusu mgogoro wa Libya, iliochapishwa kwenye magazeti nchini humo Rais Museveni amemkosoa na pia kumtetea Kanali Muamar Gaddafi.

Kiongozi huyo amepinga upinzani ambao unaungwa mkono na mataifa ya kigeni na ameyaita mataifa hayo kama yenye undumila kuwili unaothibitishwa na kuweka haraka marufuku ya ndege kupaa kwenye anga ya Libya.

Museveni ambaye ni mmoja walioteuliwa kwenye jopo la kutatua mzozo huo na Umoja wa Afrika amehoji kwa nini nchi hizo zina puuza hali mbaya kama vile ya Bahrain ama maeneo mengine yenye kuegemea upande wa magharibi.

Katika tahariri hiyo, anauliza ikiwa Benghazi pekee ndio kuna raia na Mogadishu hakuna au ni kwa sababu nchini Somalia ambapo wameomba Umoja wa Mataifa kuingilia kati mzozo unaoendelea hakuna mafuta.

Aidha, Rais Museveni amemsifu Kanali Gadafi kama mmoja wa viongozi wa Kiarabu ambae hashabikii uislamu wa itikadi kali.

Kiongozi huyo pia amemsifu Gaddafi kama kiongozi wa Afrika ambaye ana mawazo yake binafsi asie shawishika na sera za kigeni.

Kwenye tahariri hiyo pia, Rais Museveni amekosoa sera za Gaddafi, na kutoa mifano kama alivyounga mkono utawala wa Iddi Amin alieongoza Uganda tangu mwaka wa 1971 hadi 1979.

Museveni ameongeza kuwa Gadaafi alikosa kuingilia mambo ya ndani ya nchi za kiafrika, kwa mfano kwa kuwahusisha viongozi wa kijadi ama kitamaduni, kama vile wafalame na watemi katika masuala ya kisiasa.

Tahriri yake imekamilika kwa kuutaka umoja wa Mataifa kudurusu azimio lake la marufuku ya ndege kupaa kwenye anga ya Libya.

No comments:

Post a Comment