KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 19, 2011

Museveni kifua mbele uchaguzi Uganda



Upigaji Kura nchini Uganda.


Matokeo yasiyokuwa rasmi ya kura ya urais nchini Uganda yanaonyesha kuwa rais aliyepo madarakani Yoweri Museveni,yuko katika nafasi nzuri ya kunyakuwa ushindi kulitawala tena taifa hilo kwa mhula wa nne.

Bwana Museveni amekuwa madarakani kwa kipindi cha miaka ishirni na tano.


Wachunguzi wa uchaguzi huo kutoka umoja wa ulaya wameutaja kuwa wa amani lakini msemaji wa upinzani unaoongozwa na Kisa Besigye amesema kumekuwa na visa vya wapiga kura kutishiwa.


Rais Museveni akiwa kwenye foleni akisubiri kupiga kura

Mwandishi wa BBC kuhusu maswala ya Afrika mashariki anasema kiasi kikubwa cha pesa za serikali kimetumiwa kuwashawishi wapiga kura kumchaguwa tena rais museveni.

No comments:

Post a Comment