KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, December 30, 2010

Mapigano Sudan yasababisha 'vifo 100'



George Athol
Zaidi ya watu 100 wanasemakana sasa kufariki dunia katika mapigano Sudan kusini baada ya waasi kushambulia jeshi.

Ripoti za awali zilisema mapigano ya wiki hii yamesababisha vifo vya watu 16.

Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini alisema, takriban watu 39 miongoni mwa waliouawa ni raia.

Mapigano baina ya wapiganaji wanaomtii George Athor na jeshi la Sudan kusini yameanza huku eneo hilo likijiandaa kwa uhuru kutoka kaskazini kufuatia kura ya maoni iliyofanyika mwezi uliopita.

Kulingana na matokeo rasmi yaliyotangazwa na maafisa wiki hii, takriban watu asilimia 99 wamepiga kura ya kujitenga kutoka kaskazini.

Bw Athor aliamua kuanzisha mapigano mwaka jana, akidai kuwepo na udanganyifu katika uchaguzi, lakini alitia saini mwezi uliopita ya kusitisha mapigano kabla ya kura hiyo ya kihistoria.

Changamoto za kiusalama
Msemaji wa jeshi la Sudan kusini Philip Aguer alisema, wanachama 20 wa majeshi ya usalama ya Sudan kusini waliuawa, pamoja na waasi 30, na kufanya jumla ya waliouawa kufikia 105.

Wakati wa mapigano hayo, magari mawili ya jeshi yalilipuliwa na mabomu ya kutegwa ardhini karibu na mji wa Fangak katika jimbo la Jonglei.

Alisema, wafuasi wa Bw Athor walifanya shambulio hilo siku ya Jumatano na mapigano yaliendelea mpaka Alhamis.

Jonglei ni mji maarufu sana upande wa kusini.

Wakati Bw Athor akiamua kuchukua silaha, upande wa kusini ulimtuhumu kwa kutumiwa na upande wa kaskazini ili kuchochea ghasia na kuharibu kura ya maoni, tuhuma ambazo maafisa wa upande wa kaskazini unazikana

No comments:

Post a Comment