KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, November 8, 2010

Sitta atarudi bungeni? Chenge ammiminia tuhuma!

Samuel Sita
Andrew Chenge


BUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge anaonekana kumtupia vijembe spika aliyemaliza muda wake Samuel Sita, kwa kudai kuwa bunge lililoisha halikuwa makini kwa kuwa muongozaji wake alikuwa akichochea chuki na hakuwa shujaa na kuacha majeraha meng
Chenge alidai hayo jana alipokuwa akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam kwa kusema bunge lililoisha halikuwa makini kwa kuwa muongozaji alikuwa akitengeneza tuhumana kuwachafua wengine.

Hayo yamekuja ni siku chache toka mbunge huyo kuchukua fomu ya kuwania kugombea kiti hicho.

“Ni hatari kuendelea kuliacha Bunge kuongozwa na mtu ambaye ubora wake unapimwa kwa umahiri wake wa kuwapaka matope wengine” hafai chagueni watu makini,

“Mimi nina uwezo wakuendesha bunge kwa kuwa nina uzoefu wa muda mrefu serikalini, nimeshakuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa miaka 10.

Sitta aliyemaliza muda wake, katika uchaguzi huu ameshinda tena ubunge Jimbo la Urambo Mashariki, na teyari ameshachukua fomu kwa mara nyingine kutetea kiti chake

No comments:

Post a Comment