KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Korea Kusini yafuta mazoezi ya kijeshi


Serikali ya Korea Kusini imetangaza kufutiliwa mbali mazoezi ya kijeshi ambayo yangehusisha matumizi wa silaha, katika kisiwa kilichoshambuliwa na wanajeshi wa Korea Kaskazini wiki iliyopita.


Korea Kusini yafuta mazoezi ya kijeshi


Jeshi la nchi hiyo limesema mazoezi hayo ni sehemu ya mazoezi ya pamoja yanayoendelea kati ya nchi hiyo na Marekani.

Hata hivyo hakuna sababu yoyote iliyotolewa kuhusu sababu zilizosababisha harakati hizo za mazoezi ya kijeshi zifutiliwe mbali.

Utawala wa Korea Kaskazini umesema mazoezi hayo yanayohusisha ufyatuaji risasi yalichochea uamuzi wake wa kushambulia kisiwa cha Yeonpyeong island siku ya jumanne wiki iliyopita.

Rais wa Korea Kusini, Lee Myungt Bak amesema atakabiliana vikali na serikali ya Korea Kaskazini endapo itajaribu kufanya mashambulio kama hayo

No comments:

Post a Comment