KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 19, 2010

Kikwete atangaza baraza la mawaziri


Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ametangaza baraza lake jipya la mawaziri kukamilisha uundaji wa serikali tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwezi Oktoba.


Kikwete amewaacha mawaziri kadhaa wa zamani na kuteua sura mpya kama vile Profesa Anna Tibaijuka.


Rais Kikwete alitaja serikali yake mbele ya waandishi wa habari katika shughuli iliyofanyika Ikulu mjini Dar Es Salaam, akibainisha kuwa hakuna mabadiliko makubwa katika idadi ya wizara, zipo jumla ya wizara 26.

Sura mpya kadhaa zimetajwa ikiwa ni pamoja na Profesa Anna Tibaijuka atakayesimamia wizara ya ardhi na makazi.Profesa Tibaijuka alikuwa mkurugunzi mkuu wa shirika la makazi la Umoja wa Mataifa kabla ya kujiuzulu na kwenda kugombania ubunge jimbo la Muleba Kusini.

Waziri aliyetajwa kinyume na maelezo ya wachambuzi wengi wa kisiasa ni Samuel Sitta, baada ya kuondolewa kiti cha spika wa bunge la Muungano, sasa anakuwa Waziri wa maswala ya Afrika Mashariki.

Mawaziri wengi wa serikali iliyopitwa wamerejeshwa tena katika majukumu waliyokuwa nayo awali kama vile Bernard Membe atakayeendelea kusimamia mambo ya nje.Mustapha Mkullo anarudi kuongoza wizara ya fedha.

Marekebisho kadhaa ameyataja Rais Kikwete katika uundaji wa baraza lake kuwa idara ya vijana imeondolewa kutoka wizara ya kazi na kuhamishiwa wizara ya habari na michezo.

Wanasiasa kadhaa waliokuwa katika serikali iliyopita wameachwa, baadhi yao ni wasomi maarufu kama Profesa Peter Msola aliyekuwa Sayansi na Teknolojia, Profesa Juma Kapuya aliyekuwa Kazi na Profesa David Mwakyusa aliyekuwa afya, mwingine ni kada wa chama kama John Chiligati aliyeachwa wizara ya ardhi.

Waziri hao wataapishwa siku ya Jumamosi katika viwanja vya Ikulu ya Dar Es Salaam.

Orodha kamili ya mawaziri na manaibu waziri hii hapa chini.


Namba

Ofisi/Wizara

Waziri


Naibu Waziri

1.
Ofisi ya Rais
1. Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais – Utawala Bora

Mathias Chikawe

2. Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais – Mahusiano na Uratibu

Stephen Wassira

2.
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Hawa Ghasia

3.

Ofisi ya Makamu wa Rais
1. Muungano

Samia Suluhu

2. Mazingira

Dr. Terezya Luoga Hovisa

4.

Ofisi ya Waziri Mkuu

1. Sera, Uratibu na Bunge

William Lukuvi

2.Uwekezaji na Uwezeshaji

Dr. Mary Nagu

5.

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

George Mkuchika
1.Aggrey Mwanri

2. Kassim Majaliwa

6.

Wizara ya Fedha


Mustapha Mkulo
1. Gregory Teu

2. Pereira Ame Silima

7.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Shamsi Vuai Nahodha
Khamis Kagasheki

8.

Wizara ya Katiba na Sheria
Celina Kombani

9.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Bernard Membe
Mahadhi Juma Mahadhi

10.

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa


Dr. Hussein Mwinyi

11.
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. Mathayo David Mathayo
Benedict Ole Nangoro

12.

Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Charles Kitwanga

13.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi


Prof. Anna Tibaijuka
Goodluck Ole Madeye

14.

Wizara ya Maliasili na Utalii
Ezekiel Maige

15.

Wizara ya Nishati na Madini
William Ngeleja
Adam Kigoma Malima

16.

Wizara ya Ujenzi
Dr. John Magufuli
Dr. Harrison Mwakyembe


17.

Wizara ya Uchukuzi




Omari Nundu
Athumani Mfutakamba

18.

Wizara ya Viwanda na Biashara
Dr. Cyril Chami
Lazaro Nyalandu

19.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru Kawambwa
Philipo Mulugo

20.

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Haji Hussein Mpanda
Dr. Lucy Nkya

21.

Wizara ya Kazi na Ajira
Gaudensia Kabaka
Makongoro Mahanga

22.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Sophia Simba
Umi Ali Mwalimu

23.

Wizara ya Habari, Vijana na Michezo
Emmanuel Nchimbi
Dr. Fenella Mukangara

24.

Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Samuel Sitta
Dr. Abdallah Juma Abdallah

25.
Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika
Prof. Jumanne Maghembe
Christopher Chiza

26.
Wizara ya Maji
Prof. Mark Mwandosya

Eng. Gerson Lwinge

No comments:

Post a Comment