KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 6, 2010

IDARA ya Usalama wa Taifa limejibu mapigo ya tuhuma hadharani waliyotupiwa na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa



IDARA ya Usalama wa Taifa limejibu mapigo ya tuhuma hadharani waliyotupiwa na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa kwa kuwahusisha na uibaji wa kura ya matokeo ya urais.
Naibu mkurugenzi wa idara hiyo, Jackie Zoka, alikemea vikali tuhuma hizo na kumtaka mgombea huyo kuthibitisha hayo.

Zoka alimtaka Dk Slaa kutoa ushahidi wa madai yake hayo kwa kuwa asipotoa majibu wananchi wanaweza kuamini akisemacho.

Hivyo alimtaka dk. Slaa kuwa makini na watu wanaompa maneno ya uwongo mana hali hiyo inaweza ikaivuruga nchi na kumwamabia asikurupuke kuongea uwongo kabla hajayafanyia kazi maneno anayoambiwa.

Alisema idara hiyo kimsingi ni rafiki wa vyama vya siasa na iko tayari wakati wote kushirikiana navyo katika kutekeleza majukumu yao

No comments:

Post a Comment