KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Daladala kutishia kugoma Ijumaa


CHAMA cha Wamiliki wa Daladala Mkoa wa Dar es Salaam (Darcoboa), umetishia kufanya mgomo wa kutoa huduma hiyo ifikapo Ijumaa ya wiki hii endapo utaratibu wa kukamata na kuzishikilia daladala hizo isivyo halali hautasitishwa mara moja.
Hayo yalithibitishwa jana na Mwenyekiti wa Darcoboa, Bw. Sabri Mabruk jijini Dar es Salaam.

Alisema mgomo huo utakuwepo endapo askari wa barabarani wataendelea na utaratibu wa kukamata gari hizo isivyo halali na kusumbua wamiliki wa gari hizo na kuchukulia utaratibu huo ni ukandamizaji.

Alisema, trafiki wamekuwa wakikamata daladala mbalimbali na kuzipeleka kwenye ofisi za Wakala wa Umeme na Ufundi (Temesa), badala ya kituo cha polisi.

Hata hivyo aliendelea kulalamika kuwa, askari hao wamekuwa wakisumbua wamiliki hao na kuwapeleka Tamesa na kukuta madeni ya makosa tofauti yaliyofanyika nyuma na kutotambua makosa hayo uliyafanya lini na kwa kipoindi gani kwa kuwa huko unakuta namba ya gari iliyofanyakosan hilo bila kutambua.

Hivyo alisema vitendo hivyo vimeanza muda mrefu na kuvimezea mate na sasa kuonekana kuota mizizi kwa kuwa gari likikamatwa huchukua hata siku nne halijatoka na wao kukosa vipato vyao vya kila siku

Wamilika hao waliongeza kuwa utaratibu huo hawakubaliani nao kwa kuwa hauonyeshi vithibitisho ya makosa hayo na kuwakosesha uhuru

No comments:

Post a Comment