KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

Tariq Aziz sasa ahukumiwa kifo



Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Iraq, Tariq Aziz amehukumiwa adhabu ya kunyongwa.

Mahakama ya juu zaidi nchini humo ilimpata Aziz na hatia ya kuwatesa wafuasi wa vyama vya Kishia.

Aziz ambaye pia alikuwa naibu waziri mkuu amekuwa jela tangu Marekani na nchi washirika kuivamia Iraq mwaka wa 2003.




Waziri huyo wa zamani ambaye ni mwumini wa dini ya Kikristo, alijasalimisha kwa majeshi ya Marekani wakati huo.

Mwezi wa Machi mwaka huu, alihukumiwa kifungo cha miaka 15 kwa kuhusika katika mauaji ya watu 40.





Kwa muda mrefu Aziz alipata umaarufu kimataifa akiiwakilisha serikali ya Iraq na mshauri wa karibu wa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Saddam Hussein.

Taarifa zaidi zinasema ambaye Aziz anaugua kiarusi, hali yake ya afya ni dhoofu.

No comments:

Post a Comment