KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, October 30, 2010

Osama Bin Laden Agundulika Anapoishi


Kwa mujibu wa maafisa wa majeshi ya Nato, Osama bin Laden hajajificha mapangoni kama inavyojulikana bali anaishi maisha ya kifahari kwenye jumba moja la kifahari kaskazini mwa Pakistan.
Kiongozi wa Al Qaeda, Osama bin Laden hajakimbilia mafichoni kwenye mapango bali anaishi maisha ya kifahari kwenye makazi ya watu nchini Pakistan.

Msaidizi mkuu wa Osama, Ayman al-Zawahiri naye anaishi maisha ya kifahari katika nyumba nyingine iliyopo katika maeneo ambayo Osama bin Laden anadaiwa anaishi.

“Hakuna kiongozi yoyote wa Al Qaeda anayeishi kwenye mapango”, alisema afisa mmoja wa ngazi za juu wa Nato ambaye hakutaka kutaja jina lake kutokana na taarifa hizo kuwa nyeti sana.

Afisa huyo wa Nato alisema kuwa Osama bin Laden na al-Zawahiri wanalindwa na wakazi wa maeneo hayo ambao wanashirikiana vyema na majasusi wa Pakistan.

Baada ya mashambulizi ya 9/11 nchini Marekani, ilidaiwa kuwa Osama bin Laden na wadau wake wamejificha kwenye mapango ya Tora Bora yaliyopo kwenye milima iliyopo mpakani mwa Afghanistan.

Lakini sasa imedaiwa kuwa Osama amekuwa akiishi kwa kujificha katika nyumba ya kifahari iliyopo kwenye kitongoji cha Chitral kilichopo kaskazini mwa Afghanistan karibu na milima ya Tora Bora.

Taarifa ya Osama kuishi maisha ya kifahari nchini Pakistan huenda ikawaudhi maafisa wa Marekani ambao walitangaza kuwa mabomu yao yamemfanya Osama bin Laden ajichimbie kwenye mapango ya Tora Bora.

Rais wa Marekani, Barack Obama ameendelea kusisitiza kuwa wanamsaka kwa udi na uvumba Osama bin Laden ambaye amehusishwa na matukio mengi ya ugaidi katika maeneo mbalimbali duniani

No comments:

Post a Comment