KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, August 24, 2010

Wananchi Niger wataabika kwa majanga

Ukame, mafuriko na kupanda kwa bei ya chakula ni matatizo yaliyowaacha mamilioni ya raia wa Niger katika hali ya kutapatapa wakati kipindi cha mavuno yakisubiriwa miezi kadhaa.

Mfanyakazi wa shirika la misaada la nchini Niger amejitolea kusaidia wanakijiji cha Tidirra, kilichoko kusini mwa nchi.



Akitokwa jasho la jua kali ndani ya nyumba iliyojengwa kwa matofali ya udongo, Adamo Gabeye anachanganya unga wenye rangi ya dhahabu hivi na sehemu ndogo ya ufuta na vitamini.

Kwa utaratibu unaoelekea kama anayetayarisha mkate, Gabeye anachanganya ufuta na unga wa mahindi, soya na sukari.


Anayafanya hayo huku akiandamwa na akina mama 14 waliokalia viti upande mmoja wa chumba.

Vitoto vichanga vilivyopakatiwa na mama hawa vinahangaika kutafuta maziwa ingawa akina mama hawana tena uwezo wa kutoa maziwa ya kutosha. Hali hii inatishia watoto hawa wanaoonekana kama wenye upungufu mwilini.
Takwimu

Hiyo ndiyo hali iliyoko Niger mojawapo ya nchi masikini duniani, lakini kwa sasa inakabiliwa na kukosa chakula.



Mvua ya kupindukia katika sehemu za nchi mwaka uliopita iliharibu mashamba na mazao kama mawele, mtama na mahindi ikisababisha upungufu mkubwa wa mavuno na hadi mwaka huu watu wamekosa chakula.

Zaidi ya asilimia 80 ya watu wa Niger, takriban watu milioni 12 wanakabiliwa na ukosefu wa chakula. Utapia mlo ni wa kupindukia na hali hiyo imezidi viwango vya dharura.
Bei ya chakula yapanda

Serikali ya Niger imeyahimiza mashirika ya kimataifa ya misaada yanunue chakula nje ya nchi ili kuepusha kupanda kwa bei katika masoko ya ndani.

Hakuna anayekanusha kupanda kwa bei ya chakula nchini Niger. Bei ya mawele ilipanda mara dufu katika miaka ya hivi karibuni.

Kwa mujibu wa serikali, wafanyabiashara wakubwa wameshikilia biashara ya kuagiza chakula kutoka nje na hivyo kupandisha bei wanavyotaka.

Na katika chumba anakochanganya unga wenye rangi ya dhahabu na soya, ufuta na sukari Adamo anafahamu vyema kuwa watoto waliomkodolea macho watategemea mchanganyiko wa ugali anaoutengeneza ili kunusuru maisha yao





ShelterBox - Niger - Floods - September/October 2009


An initial 15 tonnes of emergency disaster relief ShelterBox aid was sent to Niger after horrific flooding in West Africa affected nearly 100,000 people in Agadez, Niger.

Tremendous efforts by ShelterBox France, working side by side with the French government and military, secured a French military C-130 aircraft to fly the aid immediately into Agadez.

In total 700 ShelterBoxes, with enough aid for up to 7,000 people was sent to Niger.






The raging waters destroyed the dyke protecting the town of Agadez, flooding entire sectors and prompting the government to call for international assistance on September 11.

While no epidemics have thus far been reported, cases of diarrheal disease and malaria are on the rise. Thousands of children under the age of five are particularly at risk of contracting infectious diseases caused by unsafe water and poor sanitation.

In response, UNICEF is now coordinating with the government, United Nations agencies and other partners to see that children and women receive access to basic services.

"It is UNICEF's priority to ensure that essential services are available at the sites for affected people, in line with its core commitments for children in emergencies. This includes access to basic health, nutrition, potable water and sanitation, education, protection and psycho-social support," said UNICEF Representative in Niger Akhil Iyer.

UNICEF is also working on disseminating lifesaving messages on good health and hygiene practices.

No comments:

Post a Comment