KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, June 29, 2010

Maonyesho ya Sabasaba kuanza leo


MAONYESHO ya 34 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika kila mwaka jijini Dar es Salaam yanaanza leo rasmi na wananchi kutakiwa kutembelea maonyesho hayo.
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, amewataka wananchi kuhudhuria maonyesho ya 34 ya Biashara ya Kimataifa yanayoanza rasmi leo.

Lukuvi alitoa wito huo jana katika viwanja vya maonyesho hayo, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya maonyesho hayo.

Maonysho ya mwaka huu yatakuwa na mabadiliko kwa kuwa yameandaliwa kwa ustadi mkubwa na kwa umakini zaidi.

Maonyesho hayo yatafunguliwa rasmi na Rais wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva.

Katika maonyesho hayo ya kibiashara ya kimataifa yanawapa fursa wanacnhi mbalimbali kujifunza mambo mbalimbali ya kitaifa ikiwemo na kununua bidhaabmalimbali zinazofika katika maonyesho hayo

Nifahamishe juzi,ilishuhudia mabanda mbalimbali yakiwa tayari kwa maonyesho hayo na mengine yakiwa katika hatua za mwisho ya maandalizi

No comments:

Post a Comment