KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, June 29, 2010

JK aja na Ari Zaidi, Nguvu Zaidi na Kasi Zaidi


RAIS Jakaya Kikwete jana wakati alipokwenda kuchukua fomu ya kuwania urais alikuja na kauli mbiu mpya ya kutetea nafasi hiyo iliyosema Ari Zaidi, Nguvu Zaidi na Kasi Zaidi hii ni katika kuboresha kauli mbiu ilioyopita ktka kutimiza ahadi zake kwa w
Rais Kikwete alisema pindi atakapochukua kiti hicho ataboresha zaidi na ameshaweka vipaumbele kumi muhimu ikiwemo kuongeza kasi ya mapambano ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Alisema vipaumbele vingine ni kuongeza jitihada na mipango zaidi ya kuwawezesha kiuchumi wananchi hasa wa hali ya chini zaidi ili waweze kushiriki na kunufaika na uchumi unaokua.

Vipaumbele vingine atahakikisha serikali ijayo itaongeza jitihada za kupanua wigo na kuboresha huduma muhimu za kijamii hasa afya na maji mbazo zimeonekana ni kero kubwa kwa wananchi walio wengi.

Pia alisema atahakikisha huduma za umeme, miundombinu na mawasiliano zitaboreshwa zaidi.

Rais Kikwete aliyasema hayo mara baada ya kuchukua fomu hiyo katika ofisini ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Bw. Yusuf Makamba aliongozana na familia yake na wadhamini wake mjini Dodoma.

Pia Kikwete alitimiza na kulipia shilingi millioni moja kama ada ya kuchukulia fomu na kuonyesha wananchi risiti waliohudhuria hafla hiyo

No comments:

Post a Comment