KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 31, 2010

Viongozi wa Asia wakutana Korea Kusini


Viongozi wa Uchina, Japan na Korea ya Kusini wamekubaliana kufanya kazi pamoja katika kusuluhisha mzozo juu ya kuzama kwa manuari ya kijeshi ya Korea ya Kusini.

Baada ya kumalizika kwa mkutano wao nchini Korea ya Kusini, viongozi wa mataifa hayo wamefanya mkutano na waandishi wa habari.

Viongozi wote watatu walikubaliana kuwa kuzama kwa manuari ya Korea ya Kusini, ambapo watu 46 walipoteza maisha yao mwezi March, ni changamoto kubwa kwa usalama na utulivu wa eneo hilo.

Waziri Mkuu wa Japan,Yukio Hatoyama, ameahidi kumuunga mkono Rais wa Korea ya Kusini, Lee Myung-bak na ameongeza kuwa anakubaliana kikamilifu na ushahidi kuwa manuari hiyo ilililipuliwa na kombora la torpedo lililofyatuliwa na nyambizi ya Korea ya Kaskazini.

Msimamo wa Uchina baado haujabainika wazi. Kwenye mkutano huo na waandishi wa habari, Waziri Mkuu wa Uchina, Wen Jiabao, alituma salamu za rambi rambi kwa familia za mabaharia waliouwawa, na akazungumzia umuhimu wa kutuliza hali ya wasiwasi iliyopo, lakini hakusema chochote kuhusu msimamo wake juu ya suala la Korea ya Kaskazini kuhusishwa na shambulizi hilo.

Utawala wa Beijing unadhaniwa kuhofia kumchokoza mshirika wake wa siku nyingi katika vita baridi duniani, huku Pyongyang ikikanusha vikali madai ya kuhusika na shambulizi la kombora dhidi ya manuari ya jirani wake, Korea ya Kusini.

No comments:

Post a Comment