KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, May 29, 2010

Jose Mourinho Atua Real Madrid

Wababe wa Hispania Real Madrid, wamefanikiwa kumnyakua kocha wa mabingwa wa ulaya Inter Milan ya Italia, Jose Mourinho.
Baada ya kutwaa makombe matatu msimu huu, kocha wa Inter Milan, Jose Mourinho ameitosa timu hiyo na kuhamia kwa timu tajiri duniani ya Real Madrid ya Hispania.

Tovuti ya Real Madrid ilitoa taarifa leo kuwa makubaliano yamefikiwa kati ya Inter Milan na Real Madrid hivyo Mourinho ndiye atakayekuwa kocha mpya wa Real Madrid.

Awali kabla ya makubaliano hayo kufikiwa, Inter Milan iligoma kumuachia Mourinho ikitaka ilipwe fidia ya euro milioni 16 kwa Mourinho kukatisha mkataba wake ambao umebakiza miaka miwili.

Rais wa Real Madrid Florentino Perez alienda Milan kukutana na mwenyekiti wa Inter Milan Massimo Moratti ili kufikia muafaka juu ya suala hilo la Mourinho. hata hivyo maafikiano yaliyofikiwa na klabu hizo hayakuwekwa wazi.

Jose Mourinho atatambulishwa kwa wapenzi wa Real Madrid siku ya jumatatu saa saba mchana kwa saa za Tz kwenye uwanja wa Real Madrid wa Santiago Bernabeu.

No comments:

Post a Comment