KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Chama cha CCJ Champa Tendwa Wiki Moja

Chama cha Jamii CCJ kimempa wiki moja msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa ahakikishe ametoa usajili wa kudumu kwa chama hicho.
Msemaji mkuu wa chama cha CCJ Fred Mpendazoe alitoa tamko hilo wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

Mpendazoe alisema kuwa mnamo tarehe 17 mei mwaka huu msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa akizungumza na waandishi wa habari alieleza kuwa Ofisi yake kwa wakati huu haina fedha za uhakiki wa wanachama wa chama cha jamii cha CCJ ili hatimaye chama hicho kiweze kupata usajili wa kudumu na kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Mpendazoe aliwambia wandishi wa habari kuwa uongozi wa chama hicho cha CCJ umesikitishwa na kauli hiyo ya msajili wa vyama hapa nchini kwani imetolewa ikionyesha nia ya wazi ya kutotaka kufanya uhakiki na hatimaye kutotoa usajili wa kudumu kwa chama hicho.

Alisema kuwa ni muhimu sana kauli hiyo iliyotolewa na msajili wa vyama isiachwe bila kutolewa majibu.

Mpendazoe alitabainisha kuwa lengo la usajili wa muda kama inavyojulikana lilikuwa ni kuwapa nafasi ya kujiandaa na usajili wa kudumu lakini hali haikuwa hivyo kwani msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ameonesha nia yake ya kutotaka kutoa usajili wa kudumu kwa chama hicho jambao ambalo ni kinyume na sheria ya usajili wa vyama.

Mpendazoe alisema kuwa ni heri wananchi wakafa wamesimama kuliko kuishi wamepiga magoti.

Mpendazoe alisema kuwa uongozi wa CCJ unampa Tendwa wiki moja ahahakishe anakipatia usajili wa kudumu chama hicho.

No comments:

Post a Comment