KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Aliyejaribu Kuulipua Ubalozi wa Marekani Afikishwa Mahakamani

MTOTO Nassib Mpamka (15) mwanafunzi wa kidato cha pili, katika shule ya Sekondari Biafra Dar es Salaam, anayekabiliwa na tuhuma za kufanya jaribio la kuulipua Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Nassib alifikishwa mahakamani hapo jana, chini ya ulinzi wa maofisa wa Polisi.

Hata hivyo mahakama hiyo haikuwa tayari kusoma mashtaka hayo kwa kudai kuwa jalada lake lilihamishiwa mahakama ya watoto na mashauri juu ya kesi hiyo hayaruhusiwi kuripotiwa na vyombo vya habari kwa mujibu wa sheria za nchi.

Mwanafunzi huyo alionekana akihamishwa kutoka mahakama ya kawaida kupelekwa mahakama ya watoto lakini baadae alirudishwa tena mahakama ya kawaida baada ya kutopatikana kwa hakimu wa kusikiliza shauri lake kwenye mahakama ya watoto.

Juhudi za wanahabari za kutaka kujua hatma ya mtoto huyo kama alisomewa mashitaka ama la hazikuzaa matunda kwa kuwa ilidaiwa kesi za watoto zinakuwa zinaendeshwa kwa usiri

Pia mujibu wa tarifa kutoka ndani ya jeshi la polisi ilidaiwa kuwa mtoto huyo alipelekwa katika mahabusu ya watoto iliyoko Upanga jijini Dar es Salaam.

Awali, Mei 16 mwaka huu, majira ya saa 2:30 usiku, Nassib Mpamka alidaiwa kufika katika maeneo ya jengo la ubalozi wa Marekani na alirusha chupa iliyokuwa imejaa mafuta ya taa iliyowekwa utambi na chupa hiyo iliangukia katika eneo ambalo lilikuwa karibu na maegesho ya malori ya kubebea maji.

Nia ya Nasibu ilikuwa ni kuyalipua malori hayo na kusababisha moto mkubwa ambao ungeuteketeza ubalozi lakini walinzi waliwahi kumkamata kabla hajarusha bomu lake la pili mafuta ya taa.

No comments:

Post a Comment