KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 6, 2010

Terry ang'olewa unahodha England




John Terry amevuliwa unahodha wa timu ya taifa ya England kutokana na madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wa mchezaji mwenzake.
Terry, mwenye umri wa mika 29, kabla ya uamuzi huo alifanya mazungumzo na kocha Fabio Capello wa England katika uwanja wa Wembley siku ya Ijumaa.

"Baada ya kutafakari kwa muda mrefu, nimeamua kwamba litakuwa jambo jema kwangu kumvua John Terry unahodha," alieleza Capello katika taarifa.

Terry mlinzi wa Chelsea ambaye amerithiwa wadhifa huo na mlinzi mwenzake Rio Ferdinand, alisema anaheshimu uamuzi wa Capello kumng'oa yeye.

No comments:

Post a Comment